Hatua 3 Muhimu Kuanza Kufanikiwa Maishani.
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Hatua 3 Muhimu Kuanza Kufanikiwa Maishani.

“Jifunze hatua tatu muhimu zinazoweza kukusaidia kuacha maisha ya kushindwa na kuanza safari ya mafanikio ya kweli. Tambua nguvu ya mawazo, maamuzi, na matendo yako kila siku”

Read More
Kustaafu Ni Mwanzo Mpya siyo Mwisho
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Kustaafu Ni Mwanzo Mpya siyo Mwisho

Ni mzee aliyeamua kuanza kuishi ndoto yake kwa kuanza mazoezi ya kujenga mwili akiwa na umri wa miaka 87.Ni mwanariadha aliyeshikilia rekodi ya ushindi wa mbio za mita 400 na 600 katika kundi la watu wa umri wake.Alishikilia rekodi za ushindi 4 mbili nchini Uingereza za dunia katika umri wa miaka zaidi ya 90. Ni mwandishi wa kitabu cha "Age is Just Numbers" alichokiandika akiwa na umri wa miaka 95.

Read More
 Kama Una Tabia Hii Unasaidia Wengine Kuishi.
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Kama Una Tabia Hii Unasaidia Wengine Kuishi.

Kwa nini mtu mmoja anafanikiwa kumiliki muda wake na kuweza kuonyesha matunda ya namna alivyotumia muda wake vizuri na wakati huo huo mwingine anahangaika namna ya kutawala na kutumia muda wake vizuri?

WATU wengi wanajua kwamba muda ni mali ingawa matendo wanayofanya hayaonyeshi kuunga mkono imani hiyo, na imani bila matendo ni sawasawa kabisa na mtu asiyeamini bado kitu chochote.

Read More
Namna Ya Kushinda Tabia Ya Kuahirisha Mambo
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Namna Ya Kushinda Tabia Ya Kuahirisha Mambo

Azimio la kujenga makazi ya kudumu ili kuepuka maumivu yanayosababishwa na hali ya majira kubadilika lilipitishwa tangu enzi za mababu na mababu, lakini limeahirishwa mpaka leo. Siyo babu wala baba zake waliofaulu kutimiza azma ya kujenga makazi ya kudumu.

Jitihada za kujikinga na kukinga watoto wake dhidi ya mvua kali iliyokuwa inanyesha wakati mwingine ziligonga mwamba na kujikuta kila mmoja katika familia ya manyani akihangaika kujitafutia namna ya kujizuia na mvua kali iliyokuwa inanyesha. 

Read More
Maisha Ni Mradi Wako Mwenyewe!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Maisha Ni Mradi Wako Mwenyewe!

“Maisha ni mradi wa kufanya wewe mwenyewe (life is a do yourself project)” ni msemo na nukuu ya Napolion Hill kupitia kitabu chake maarufu cha Think and Grow Rich alipokuwa anasisitiza juu ya umuhimu wa kila binadamu kutimiza wajibu wake kuhakikisha  anafikia kusudi la kuwepo kwake hapa duniani.

Read More
Kwa Nini Wengi Hushindwa Kuishi Ndoto Zao!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Kwa Nini Wengi Hushindwa Kuishi Ndoto Zao!

Kuna tofauti kubwa kati ya mtu anayejua anachotaka kufanya ambaye huthubutu kufanya bila woga na yule ambaye yeye licha ya kujua anapashwa kufanya nini lakini anakosa ujasiri kufanya kwa kuongozwa na hali ya hofu na kusitasita.

Read More
Kazi Ni Nyingi, Ajira Chache!!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Kazi Ni Nyingi, Ajira Chache!!

Ingawa watu wengi wanajua kuwa ulimi huumba na mara nyingi kinywa hukiri kile kinachoujaza moyo,hawaachi kukiri na kujitamkia misemo ambayo imezoeleka katika maisha yao na matokeo yake wanaanza kuiishi. Miongoni mwa misemo hiyo ni pale unaposikia watu wanakiri kuwa hakuna kazi siku hizi na kwa kuwa ndivyo wanavyoamini basi,hivyo ndivyo inavyokuwa kwao na nafasi za kazi zinakuwa adimu kweli kweli.

Read More
Namna Nzuri Ya Kutafuta kazi
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Namna Nzuri Ya Kutafuta kazi

Hakuona sababu ya kubweteka kwa sababu alikuwa anatoka katika familia tajiri,badala yake alipita mtaani kutafuta kitu cha kufanya bila kujali kwamba yeye ni msomi wa chuo kikuu aliyehitimu katika fani ya uchumi na utawala.

Read More
Maneno Bila Matendo Haitoshi!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Maneno Bila Matendo Haitoshi!

“Nitalima maharage mengi sana na mahindi katika shamba hili.Siku ya kuuza mazao yangu hakuna mkulima mwingine atakayepata nafasi ya kuuza,kuanzia asubuhi mpaka muda wa kufunga soko nitauza mazao yangu tu” alisisitiza

Read More
Muhimu Ni Mwisho Siyo Mwanzo!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Muhimu Ni Mwisho Siyo Mwanzo!

Kuna mafundi wengi vijana na watu wazima waliopita mikononi mwake ambao wale waliotimu kufuata maelekezo yake kwa kufanya kazi kwa ubora wa wa hali ya juu, uaminifu na kujituma ilimtofautisha sana na mafundi wengi wa aina yake kijijini kwao na maeneo yaliyozunguka kijiji chao.

Read More
Kitu Hiki Kila Mtu Anacho!!!
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Kitu Hiki Kila Mtu Anacho!!!

Kuna kitu kimoja pekee hapa duniani ambacho Mungu amempa kila mtu bila upendeleo ni muda. Kufanikiwa au kutokufanikiwa kwa mtu kunategemea sana namna anavyotumia muda wake.

Read More
Namna Ya Kupata Fursa Ya Biashara
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Namna Ya Kupata Fursa Ya Biashara

Watu wengi wanatamani kuwa wajasiliamali lakini changamoto kubwa inayowakwamisha ni kutokua na uwezo wa kubuni wazo la biashara.Watu wanaofanikiwa kila watakakokwenda ni wale wenye uwezo wa kutazama tofauti na watu wengine wanavyotazama na kupata fursa katikati ya kile wengine wanachoita matatizo.

Read More
Jifunze Kusema Hapana Itakusaidia…
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Jifunze Kusema Hapana Itakusaidia…

Jifunze kusema hapana mahali unapopaswa kusema hapana na ndio mahali unapopaswa kusema ndiyo.Kamwe usijaribu kusema ndiyo wakati moyoni mwako unajua kabisa ulipaswa kusema hapana na kadhalika usiseme ndiyo mahali ambapo ulipaswa kusema hapana.

Read More
Usidharau Mwanzo Mdogo
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Usidharau Mwanzo Mdogo

Kila kazi au biashara unayotaka kufanya ni muhimu kukumbuka kwamba unahitajika angalau uwe na maarifa ya msingi ya kukuwezesha kufanya biashara hiyo.Maarifa hayo yanaweza kuwa umeyapata kutoka shuleni au hata kutokana na uzoefu wa muda fulani ukifanya au ukimsaidia mtu.Maarifa yanakuwezesha kujua mazuri na mabaya yaliyo ndani ya fursa hiyo ya kufuga kuku.Kipengenere hicho ukikiruka unaweza ukapata hasara kwanza kabla ya kuingia kupata faida.

Read More
Madhara Ya Mtazamo
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Madhara Ya Mtazamo

Ikiwa unataka kufanikiwa katika eneo lolote maishani mwako unapaswa kwanza kujifunza namna ya kufikiri vizuri,kwa sababu pengo kati ya watu waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa,lipo katika namna wanavyofikiri (mtazamo) 

Read More
Tofauti Ya Kazi Na Wito
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Tofauti Ya Kazi Na Wito

Umewahi kujiuliza kuna tofauti gani kati ya wito na kazi? Ingawa watu wengi wanachanganya maana ya maneno haya mawili muhimu katika maisha na kujikuta wanazungumzia wito mahali pa kazi na kuzungumzia kazi mahali pa wito,ipo tofauti kubwa kati ya kazi na wito.

Read More
Badili Uchungu Kuwa Wito
Maisha Ni Fursa Maisha Ni Fursa

Badili Uchungu Kuwa Wito

Umewahi kumsamehe mtu aliyekukosea bila kuangalia ukubwa wa kosa alilokufanyia hata kama anaendelea kukukosea?. Mwezi wa pili mwaka 1993 Marry Johnson alipokuwa kazini alipokea simu yenye taarifa mbaya ikimjulisha kuhusu kifo cha mwanaye wa pekee Laramiun Bry ambaye alikuwa ameuawa kikatiri na muuaji Oshea Israel  huko nchini Marekani.

Read More